Skip to main content

UINGEREZA YAMLILIA MWANAMFALME PHILIP

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A"





 

Mwanamfalme Philip akiwa na mkewe Malkia Elizabeth II wakati wa uhai uhai wake.


MWANAMFALME Philip ambaye pia ni mume wa Malkia Elizabeth II amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 99.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kasri ya Buckingham kwa niaba ya Malkia imeelezwa  kuwa, "Kwa masikitiko Malkia anatangaza  kifo cha mumewe kipenzi,  Mwanamfalme Philip mtawala wa Edinburgh aliyefariki dunia kwa amani leo asubuhi Katika kasri ya Windsor Castle."

Mwanamfalme Philip alimuoa binti mfalme Elizabeth mwaka 1947 kabla ya kuwa Malkia miaka mitano baadaye na kuwa Malkia aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Uingereza.

Mwanamfalme Philip alipata heshima kutoka kwa watu wengi kutokana na kujitolea na kumuunga mkono mkewe Malkia Elizabeth II katika kazi zake, na malkia alipenda  kumwelezea mumewe kwa maneno mawili ya  'Strength and Stay.'

Viongozi mbalimbali wametuma salamu za rambirambi kwa familia huku Waziri mkuu wa Taifa hilo Boris Johson akimwelezea Mwanamfalme Philip kuwa ni jasiri aliyeongoza familia ya kifalme na ufalme kwa upendo wa hali ya juu.

Comments

Popular posts from this blog

8 Most Beautiful Brazilian Actresses

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Na Yohanec Chang'a- Iringa Brazilian women are like the sun: bright, positive, and so dang hot. It’s especially evident when you look at the models, actresses, and other juicy celebs. These women have used their immense sexuality and became the standard of beauty for men around the world. Here are the eight most beautiful Brazilian actresses. 1. Vivianne Pasmanter Vivianne’s parents dreamed that their daughter would do ballet professionally, but the girl did not like that idea and instead wished to become an actress. And she did it. Now Pasmanter can, without exaggeration, be called one of the most famous actresses on Brazilian TV series such as “Nuovo Mundo” and “Alén, Luz de Luna.” 2. Christine Fernandes Although Christine was born in Chicago, Illinois, the future actress returned to her parents’ historical homeland in Brazil at the age of three. She came to the film industry from the modeling business and almost immediately s...

NJIA YA MSALABA

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Tufwate njia ya msalaba, . Tuifuwate, mpaka Kalvario. Tusimamepo, bila haya. Msalaba, Msalaba uponya roho. Sala mbele ya Altare. Ee Mkombozi wangu, ninakuja Leo kufuata njia ile uliyoshika siku ya kufa sadaka yetu. Nimetubu dhambi zangu zote; ninataka kugeuza mwendo wangu, ninaomba kwako niwapatie roho za waumini marehemu waliomo toharani, rehema zote zilozotolewa na kanisa kwa Njia ya Msalaba. Nawe Maria Bikira Mtakatifu, uliyefuata njia ile nyuma ya mwanao Yesu, uniangalie kwa wema, unitie moyo mkuu, nisipende dhambi tena, nikivumilia kàzi na usumbufu na mateso na matukio yatakayonipata. Umekosa nini we Yesu, Kushitakiwa bure kwa Pilato, Wenye kustahili hukumu, Si wewe, si wewe Bwana ni sisi. KITUO CHA KWANZA. Yesu anahukumiwa afe. -Ee Yesu tunakuabudu, tunakushukuru. -Kwa kuwa umewakomboa watu kwa msalaba wako mtakatifu. Pilato anamhukumu Yesu ingawa haoni kosa lake, anawaogopa Wayahudi. Anabembeleza urafiki wa Kaysari. Ee Yesu ...

PETER MSECHU NATAKA NIONGEE NA WEWE KAKA KUHUSU TUNGO ZAKO KWA HAYATI MAGUFULI

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" WAKATI bado tunaomboleza msiba mzito wa Taifa wa kuondokewa na Mpendwa wetu, Aliyekuwa Rais wa Taifa letu la Tanzania, Mpenda Amani, Mpenda watu wake hususani wale wenye hadhi ya chini na kipato kidogo, Mpenda Maendeleo, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Kaka Peter Msechu naomba niongee na wewe kitu katika Tasnia yako ya Muziki... Kiukweli baada ya kutangazwa Kifo cha Hayati Dkt. Magufuli Machi 17, 2021 na Aliyekuwa Makamu wa Rais kipindi hicho, Mama Samia Suluhu Hassan, Wasanii wengi nchini walijitokeza kutunga tungo (Nyimbo) mbalimbali kumuenzi Mpendwa wetu aliyetangulia mbele ya haki. Tumeona tungo nyingi zilizojaa wasifu wakumuenzi Hayati Dkt Magufuli, tungo hizo kutoka kwa Wasanii hao wa Tanzania na Vikundi mbalimbali vya Muziki ziliwavutia watu wengi kutokana na kubeba ujumbe wa kweli kwa Taifa letu. Tumeona vikundi kama Tanzania One Theatre (TOT), Vikundi kutoka Makanisa mbalimbali nchini na Wasanii wa Muziki wa kizazi ...