Skip to main content

Tendo la baadhi ya waamini kuoshwa miguu.

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A"
Na Padre Kelvin Onesmo Mkama, Parokia ya Buhingo, Jimbo Kuu la Mwanza
Tukio hili hufanyika siku ya Alhamisi Kuu wakati wa Misa ya Karamu ya Bwana. Tukio hili hufanywa ili kukumbuka tukio la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake wakati wa Karamu ya Mwisho. Kutokana na Israeli kuwa nchi yenye joto kali mara nyingi miguu iliwaka moto na kutoa jasho jingi lililosababisha miguu kutoa harufu mbaya.
Tendo la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake lilikuwa na maana kubwa tatu:
(i) Kuonesha roho ya utumishi. Kwa tendo hili Yesu anafundisha kuwa kiongozi/mkubwa kwa hadhi anapaswa kujishusha na kuwatumikia wale anaowaongoza. Viongozi hawapaswi kubaki juu kama matawi ya miti bali wanapaswa kushuka chini kama mizizi ya miti na kuwatumikia watu. Wazazi kadhalika wanapaswa kujibidiisha kutumikia familia zao.
(ii) kuonesha roho ya unyenyekevu. Ni tendo la unyenyekevu mkubwa sana bwana kujishusha na kuosha miguu ya watumwa/watumishi wake. Kazi ya kuosha miguu ilikuwa ni kazi duni sana kuliko zote miongoni wa Wayahudi. Hivyo kwa tendo hili Kristo anajinyenyekesha na kuonekana kama mtumwa ambaye anaosha miguu. Hata Maandiko Matakatifu yanadokeza hali hii ya Kristo kujifanya mtumwa inatuonesha kuwa sisi nasi tunapaswa kujishusha katika maisha na hata kutimiza kazi zile ambazo zinatazamwa kuwa kazi duni. Tusiwe watu wa kujikweza na wenye majivuno bali wanyenyekevu kwa mfano wa Kristo mwenyewe.
(iii) dokezo juu ya Sakramenti ya Upatanisho. Tendo la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake ni kiashiria cha umuhimu wa Sakramenti ya Kitubio. Kukataa kwa makusudi Kristo atuoshe uovu/dhambi zetu kunatufanya tusiwe na ushirika naye: dhambi zetu zinatufanya tusiwe na ushirika na Kristo. Kadhalika, Yesu ametupa jukumu la kutawadhana sisi kwa sisi: Hivyo, kwa nafasi ya kwanza Mapadre wanapaswa kuwatawadha waamini wao kwa sakramenti ya Kitubio na Upatanisho na kwa nafasi ya pili, sisi sote tunapaswa kutawadhana maovu yetu sisi kwa sisi kwa njia ya kuonyana kidugu, kwa njia ya kukemea uovu na kwa njia ya kuombeana wongofu. Tusiwe kwa kwanza kuhukumu.
Uwe na maandalizi mema ya Pasaka.

Comments

Popular posts from this blog

8 Most Beautiful Brazilian Actresses

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Na Yohanec Chang'a- Iringa Brazilian women are like the sun: bright, positive, and so dang hot. It’s especially evident when you look at the models, actresses, and other juicy celebs. These women have used their immense sexuality and became the standard of beauty for men around the world. Here are the eight most beautiful Brazilian actresses. 1. Vivianne Pasmanter Vivianne’s parents dreamed that their daughter would do ballet professionally, but the girl did not like that idea and instead wished to become an actress. And she did it. Now Pasmanter can, without exaggeration, be called one of the most famous actresses on Brazilian TV series such as “Nuovo Mundo” and “Alén, Luz de Luna.” 2. Christine Fernandes Although Christine was born in Chicago, Illinois, the future actress returned to her parents’ historical homeland in Brazil at the age of three. She came to the film industry from the modeling business and almost immediately s...

8 Things You Should NEVER Say In A Relationship, Unless You Want To Break Up

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Words are a powerful instrument that can either lift you up or bring you down in a matter of seconds. Naturally, we are open to our partners and everything they have to say. Likewise, our loved ones are most sensitive to our remarks, comments, criticism, and other modes of communication that are less pleasant. Being in a relationship, you really need to filter what you say and how you say it as the damage caused by a few simple phrases can often be irreversible, causing problems for years to come. Here are 8 things you should never say in a relationship, unless you want to break up. ‘ You Don’t Know Anything’ This phrase might have been harmless for Jon Snow, but for us non-fictional beings those words sting like a bee. Even if you’re arguing, this phrase doesn’t do anything good – it just diminishes your partner’s intelligence and cripples his self-worth. If you feel that your partner doesn’t quite understand the issue, it’s best t...

SALA KWA MAMA MARIA

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Tunaukimbilia, ulinzi wako mzazi Mtakatifu wa Mungu, usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe kila siku tuingiapo hatarini, Ee Bikira Mtukufu mwenye baraka, Amina.. #MotherMary #Subscribe #Like #Comment #Share