Skip to main content

Tendo la baadhi ya waamini kuoshwa miguu.

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A"
Na Padre Kelvin Onesmo Mkama, Parokia ya Buhingo, Jimbo Kuu la Mwanza
Tukio hili hufanyika siku ya Alhamisi Kuu wakati wa Misa ya Karamu ya Bwana. Tukio hili hufanywa ili kukumbuka tukio la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake wakati wa Karamu ya Mwisho. Kutokana na Israeli kuwa nchi yenye joto kali mara nyingi miguu iliwaka moto na kutoa jasho jingi lililosababisha miguu kutoa harufu mbaya.
Tendo la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake lilikuwa na maana kubwa tatu:
(i) Kuonesha roho ya utumishi. Kwa tendo hili Yesu anafundisha kuwa kiongozi/mkubwa kwa hadhi anapaswa kujishusha na kuwatumikia wale anaowaongoza. Viongozi hawapaswi kubaki juu kama matawi ya miti bali wanapaswa kushuka chini kama mizizi ya miti na kuwatumikia watu. Wazazi kadhalika wanapaswa kujibidiisha kutumikia familia zao.
(ii) kuonesha roho ya unyenyekevu. Ni tendo la unyenyekevu mkubwa sana bwana kujishusha na kuosha miguu ya watumwa/watumishi wake. Kazi ya kuosha miguu ilikuwa ni kazi duni sana kuliko zote miongoni wa Wayahudi. Hivyo kwa tendo hili Kristo anajinyenyekesha na kuonekana kama mtumwa ambaye anaosha miguu. Hata Maandiko Matakatifu yanadokeza hali hii ya Kristo kujifanya mtumwa inatuonesha kuwa sisi nasi tunapaswa kujishusha katika maisha na hata kutimiza kazi zile ambazo zinatazamwa kuwa kazi duni. Tusiwe watu wa kujikweza na wenye majivuno bali wanyenyekevu kwa mfano wa Kristo mwenyewe.
(iii) dokezo juu ya Sakramenti ya Upatanisho. Tendo la Yesu kuwaosha miguu wanafunzi wake ni kiashiria cha umuhimu wa Sakramenti ya Kitubio. Kukataa kwa makusudi Kristo atuoshe uovu/dhambi zetu kunatufanya tusiwe na ushirika naye: dhambi zetu zinatufanya tusiwe na ushirika na Kristo. Kadhalika, Yesu ametupa jukumu la kutawadhana sisi kwa sisi: Hivyo, kwa nafasi ya kwanza Mapadre wanapaswa kuwatawadha waamini wao kwa sakramenti ya Kitubio na Upatanisho na kwa nafasi ya pili, sisi sote tunapaswa kutawadhana maovu yetu sisi kwa sisi kwa njia ya kuonyana kidugu, kwa njia ya kukemea uovu na kwa njia ya kuombeana wongofu. Tusiwe kwa kwanza kuhukumu.
Uwe na maandalizi mema ya Pasaka.

Comments

Popular posts from this blog

8 Most Beautiful Brazilian Actresses

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Na Yohanec Chang'a- Iringa Brazilian women are like the sun: bright, positive, and so dang hot. It’s especially evident when you look at the models, actresses, and other juicy celebs. These women have used their immense sexuality and became the standard of beauty for men around the world. Here are the eight most beautiful Brazilian actresses. 1. Vivianne Pasmanter Vivianne’s parents dreamed that their daughter would do ballet professionally, but the girl did not like that idea and instead wished to become an actress. And she did it. Now Pasmanter can, without exaggeration, be called one of the most famous actresses on Brazilian TV series such as “Nuovo Mundo” and “Alén, Luz de Luna.” 2. Christine Fernandes Although Christine was born in Chicago, Illinois, the future actress returned to her parents’ historical homeland in Brazil at the age of three. She came to the film industry from the modeling business and almost immediately s...

Mkuu wa Majeshi asimulia neno la mwisho kuambiwa na JPM ‘sijisikii vizuri” (+video)

SHARE TWEET SHARE SHARE COMMENTS Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ataitwa pia Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania na sio Amirat kama ambavyo ilipendekezwa. “Nashukuru Baraza la Kiswahili limerekebisha uendelee kuitwa Amiri Jeshi Mkuu na sio Amirat kama ilivyokuwa inapendekezwa”  Mabeyo Mabeyo ametoa kauli hiyo kwenye Uwanja wa Magufuli Chato leo wakati akitoa salamu kwenye Misa Takatifu ya Mazishi ya Hayati Dr.John Pombe Magufuli. RELATED ITEMS TZA HABARI SHARE TWEET SHARE SHARE COMME

Sala kwa Mama Bikira Maria

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Sala kwa Mama Bikira Maria. Salamu, Maria, umejaa Neema Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na sasa ya kufa kwetu, Amina. Utuombee kwa mwanao Yesu Kristo. #SalamuMaria #SalaniSilaha