Skip to main content

MGOMBEA AANZA KAMPENI AKIWA NDANI YA JENEZA

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A"




Na mr Camel, Yohanec chang'a TV

MWANASIASA Maarufu nchini Mexico  Carlos Mayorga ameingia katika mijadala mbalimbali baada ya kuzindua kampeni zake za Ubunge akiwa ndani ya jeneza France24 imeripoti.

Carlos Mayorga alitumia njia hiyo kuonesha hali halisi ya taifa hilo ambalo mamia ya watu wanakufa kutokana na virusi vya Corona pamoja na vurugu zinazohusiana na biashara.

Akiwa mgombea kutoka chama cha Encuentro Salidario kusini mwa jimbo la Chihuahua Mayorga alisema, alifikia uamuzi huo kwa malengo ya kufikisha ujumbe kwa wanasiasa ambao wanasababisha watu kupoteza maisha kutokana na kutojali kwao.

Mwanasiasa huyo aliwasili katika kampeni zake katika daraja linalotengenesha mji wa wa Ciudad Juarezy na El Paso Texas akiwa ndani ya jeneza la rangi ya fedha.

 Carlos Mayorga aliambatana na wasaidizi waliovaa mavazi na vifaa vya kujilinda wakiwa na mashada ya maua kama ishara ya kupaza sauti juu ya janga hilo ambapo hadi sasa watu 200,000 wamefariki nchini humo kutokana na Covid-19.

Vyombo vya habari vilimnukuu mwanasiasa huyo akisema;

"Wanasiasa wameendelea kukaa kimya wakati matukio ya uhalifu yakiendelea, na wameendelea kukaa kimya kuhusu hali mbaya ya Covid-19." Alinukuliwa.

Zaidi ya watu 300,000 wameuawa nchini Mexico tangu Serikali itoe nguvu kwa jeshi katika kupambana na vita dhidi ya dawa za kulevya 2006 kwa mujibu kwa taarifa rasmi.

Comments

Popular posts from this blog

8 Most Beautiful Brazilian Actresses

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Na Yohanec Chang'a- Iringa Brazilian women are like the sun: bright, positive, and so dang hot. It’s especially evident when you look at the models, actresses, and other juicy celebs. These women have used their immense sexuality and became the standard of beauty for men around the world. Here are the eight most beautiful Brazilian actresses. 1. Vivianne Pasmanter Vivianne’s parents dreamed that their daughter would do ballet professionally, but the girl did not like that idea and instead wished to become an actress. And she did it. Now Pasmanter can, without exaggeration, be called one of the most famous actresses on Brazilian TV series such as “Nuovo Mundo” and “Alén, Luz de Luna.” 2. Christine Fernandes Although Christine was born in Chicago, Illinois, the future actress returned to her parents’ historical homeland in Brazil at the age of three. She came to the film industry from the modeling business and almost immediately s...

Mkuu wa Majeshi asimulia neno la mwisho kuambiwa na JPM ‘sijisikii vizuri” (+video)

SHARE TWEET SHARE SHARE COMMENTS Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ataitwa pia Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania na sio Amirat kama ambavyo ilipendekezwa. “Nashukuru Baraza la Kiswahili limerekebisha uendelee kuitwa Amiri Jeshi Mkuu na sio Amirat kama ilivyokuwa inapendekezwa”  Mabeyo Mabeyo ametoa kauli hiyo kwenye Uwanja wa Magufuli Chato leo wakati akitoa salamu kwenye Misa Takatifu ya Mazishi ya Hayati Dr.John Pombe Magufuli. RELATED ITEMS TZA HABARI SHARE TWEET SHARE SHARE COMME

Sala kwa Mama Bikira Maria

#subscribe on youtube "YOHANEC CHANG'A" Sala kwa Mama Bikira Maria. Salamu, Maria, umejaa Neema Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na sasa ya kufa kwetu, Amina. Utuombee kwa mwanao Yesu Kristo. #SalamuMaria #SalaniSilaha