Skip to main content

Posts

Madhara ya kukaa, kubana mkojo kwa muda mrefu

*lackstar tours and safaris.*   3/05/2021 09:30:00 PM        makala     Utakubaliana na mimi kwamba, kitendo cha mtu kubanwa na haja ndogo siyo kitu cha hiyari kwamba sasa mtu anaamua ngoja nibanwe na mkojo, hili ni jambo la asili na ni matokeo ya vyakula, matunda au vinywaji tunavyotumia. Kwa lugha nyingine tumekuwa tukiita kuwa ni wito wa asili au nature’s call. Yawezekana mtu akawa katika mkutano, safarini, akawa katika mitandao ya kijamii anachati au popote pale akiwa anafanya jambo fulani na kutokana na jambo hilo, mtu akaendelea kujibana na kutokwenda kuyapunguza maji haya kutoka katika kibofu cha mkojo kwa kutoa kipaumbele kwa shughuli anayoifanya kuliko kusikiliza kwanza wito huu wa asili. Mambo haya tunayafanya sana, utasikia, mkojo umenibana kweli, ila ngoja nimalizie hii kazi halafu niende kujisaidia, hivi ndivyo watu wengi wanafanya. Kutokana na vyakula na vinywaji tunavyotumia, kibofu cha mkojo huanza kujaa mkojo, mkojo unapofiki...

Mwanafunzi darasa la tatu ajinyonga Njombe

*lackstar tours and safaris.*   4/13/2021 11:00:00 AM     YOU MAY LIKE Kasino bora mkondoni nchini Tanzania. Jisajili na kucheza sasa! PariMatch Kujiunga PariMatch casino sasa! Zaidi ya wachezaji milioni moja PariMatch How To Travel To U.S.A. Without A Visa? Dinnerana 6 Royal Moments That Shocked The World Brainberries Mwanafunzi wa Darasa la tatu shule ya Msingi Ikelu Makambako mkoani Njombe, Claud Frolence (9) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia kikoi akiwa anacheza na wenzake shambani.  Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Hamisi Issa amesema mwanafunzi huyo alikwenda shambani na wazazi wake na wadogo zake watatu akiwa huko walinza kucheza na wadogo zake na baadae kuchukua kikoi na kuanza kucheza michezo ya kujaribu namna ya kujinyonga. Aidha kamanda Kamanda Issa amewataka wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao kwani malezi ya Watoto ni pamoja na kuangalia aina ya michezo wanayoicheza na katika mazingira  yanayofaa.  

NITAMTAFUTA MAGUFULI MIOYONI MWA WATANZANIA,SIYO KWENYE KABURI LAKE PALE CHATO

*lackstar tours and safaris.*  AT  SUNDAY, MARCH 28, 2021     HABARI,   MAKALA, Hayati Dkt John Pombe Magufuli enzi za uhai wake.   na yohanec chang'a TV NIANZE na kipi? Mtetemo wa sauti ya Mama Samia Suluhu Hassan akitangaza kifo chake au mshtuko wa watanzania baada ya kusikia hatunaye tena? Au nianze na wingi wa marais na viongozi wa nje walioshiriki mazishi yake? Labda nianze na umati wa watanzania waliojitokeza kila kituo alichopitishwa kwa ajili ya kuagwa, Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza au Zanzibar? Sielewi nianze na kipi. Pengine nianze na idadi ya watu waliopoteza maisha yao kutokana na msiba wake. Mapenzi yao kwake ndio yaliyosababisha wapoteze maisha yao. Inasisimua kwa kweli. Ni nani huyu ninaemzungumzia? Mwanamajumui na Mwanamapinduzi halisi wa Afrika, Kiongozi mwenye haiba ya uongozi, Jiwe, Mcha Mungu na Jasiri halisi. Namzungumzia mtoto aliyezaliwa kwenye tumbo la Mama wa Kiafrika pale Chato, Geita Tanzania. Mtoto wa Mzee Joseph na Mama Suzan. M...

KUMBUKIZI YA MIAKA 37 YA KIFO CHA EDWARD MORINGE SOKOINE ALIYEFARIKI KWA AJALI YA GARI 1984 AKIWA WAZIRI MKUU WA TANZANIA

*lackstar tours and safaris.*  AT  MONDAY, APRIL 12, 2021     HABARI,   MAKALA,   MATUKIO,   Na Mzee wa Atikali ✍️ ✍️✍️ "April 12, 1984 ilikuwa ni siku mbaya sana kwa Taifa la Tanzania. Ni siku ambayo hatutaisahau kwani siku hiyo tulimpoteza Kiongozi wetu tuliyempenda sana aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. Edward Sokoine. Mh. Sokoine alifariki kutokana  na ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Wami- Dakawa". ATILIO TAGALILE, April 11, 2011 (The Citizen, Tafsiri yangu.) 1. Usuli Jumatatu ya leo, April 12, 2021, Taifa letu linatimiza miaka 37 toka marehemu EDWARD MORINGE SOKOINE, mmoja wa viongozi  bora kabisa kuwahi kutokea nchini, afariki kwa ajali ya gari Aprili 12, 1984 eneo la Dakawa, wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro.  Miaka 37, kwa umri wa mwanadamu, ni mingi sana. Hivyo, kuna baadhi ya "Bongolanderz" , hasa wa "Dot.com generation", ambao hawamjui kabisa na wengine wanamjua kijuujuu tu marehemu SOKOINE ndio maana mwandishi Bi HELLEN MATA...